282 UKIONA kiu sana ujalivu

 282

1. Ukiona kiu sana ujalivu wa Mwokozi, roho yake safi pia, liamini neno la babako na atakujazi, nawe utashangilia.

Pambio:
Atakujaliza hata utashiba. Bwana Yesu akuita: “Njoo bila ‘sitasita!” Atakujaliza hata utashiba Roho na uwezo wake.

 

2. Vichukue vyombo vyako, uvioshe safi sana kisimani pa Golgotha! Afadhali kujitoa lote kwa Mungu Bwana, na imani itaota.

 

3.Na mafuta ya neema hayakomi. Asifiwe! Tunakuwa na shukrani! Anataka kumimina Roho ya ahadi yake. Mpokee kwa imani!

Leila Morris, 1922
Are you looking for the fulness, R.H. 214