281. YOTE ninayo niliyapokea kwa wema wake

 281

1. Yote ninayo niliyapokea kwa wema wake unaonea. Namsifu Yesu, namtegemea, aliniokoa kwa neema.

Pambio:
Niliyekuwa nimetoroka, kwa pendo lake nimeokoka. Yesu yu mwema na mwenye rehema, nimeokolewa kwa neema!

 

2. Nilitembea zamani dhambini katika njia ya kufa, lakini Yesu alinitafuta porini, akaniokoa kwa neema.

 

3. Natakasiwa na Yesu Mwokozi, si kwa majuto na si kwa machozi, bali kwa damu, ninao ‘kombozi; nimeokolewa kwa neema.

 

4. Raha ya mbingu imeniingia, kwa shangwe kubwa ninafurahia Yesu, kwa kuwa anirehemia; nimeokolewa kwa neema.

J.M. Gray, 1905 Otto Witt, 1922
Naught have I gotten, RS. 605