280. JINA lake Yesu linadumu

280

1. Jina lake Yesu Kristo linadumu siku zote; jina hili la milele haliwezi kunyauka; linafaa watu wote, na wazee na vijana; linaweza kuongoza kila mtu kwake Mungu.

Pambio:
Jina hili nalipenda, limewasha moyo wangu; na kwa jina hili jema nimepata kuokoka.

 

2. Jina hili linavuma pande zote za dunia, na kwa wote linaleta tumaini na faraja. Jina hili laondoa uadui na ubaya, hata milki ya Mwokozi itaanza kutawala.

 

3. Na katika giza huku jina hili linang’aa, laonyesha msafiri njia wazi ya uzima. Jua likitiwa giza, jina hili linadumu; na milele lisifiwe hapa na mbinguni juu.