278. NINAINUA macho yangu ka Mungu

278

1. Ninainua macho yangu kwa Mungu aketiye juu, aliye msaada wangu, njiani pangu nuru kuu. Aliyefanya yote, maombi huyasikia. Katika njia zangu zote atanilinda pote pia.

 

2. Bwanangu asiache tena mguu wangu usogezwe, kwa kuwa ni mlinzi mwema, naye hatasinzia kamwe. Alinda roho yangu nisije nikapotea. Hitaji za maisha yangu baraka yake ya’enea.

 

3. Aniokoa na uovu, na roho yangu imepona. Kwa yeye nguvu na wokovu, nilizionja naku’ona. Ananilinda pote: kutoka na kuingia; anijaliza mema yote hata nakutumainia.

J. Arrhenius, 1694