277. NITAOGOPA nini gizani duniani
277
1. Nitaogopa nini gizani duniani? Sikuachiwa peke’ mbali ya tumaini! Mwokozi yu karibu, asiyebadilika.
:/: Hutunza ndege ndogo na mimi kadhalika:/:
Pambio:
Namshukuru Mungu asiyebadilika. Hutunza ndege ndogo na mimi kadhalika.
2. “E’ usifadhaike moyoni mwako, mwana”, anong’oneza Yesu, “Nitegemee sana!” Na hapo woga wangu waruka kwa hakika.
:/: Hutunza ndege ndogo na mimi kadhalika:/:
3.Na nikijaribiwa na jua lifichwapo, hata sioni raha, wala faraja hapo, nakimbilia Yesu, na yote yapinduka.
:/: Hutunza ndege ndogo na mimi kadhalika:/:
Mrs. C.D. Martin