275 E’MUNGU mwenye haki

275

1. E’ Mungu mwenye haki, uniongoze huku katika mambo yote yanayokupendeza! Nikiwa huku bila wewe, vitisho hofu na mashaka yananitia tetemeko mpaka kufa.

 

2. Ni heri siku zote kutegemea Yesu na kuenenda sawa katika nyayo zake, kwa kuwa yeye ni Mchunga anayeniongoza vema, nipate kuingia katika raha yake.

 

3. Safari yangu sasa yaelekea mbingu, Mwokozi yuko huko, lazima nifikeko na siku nitakapofika ‘tashangilia kwa furaha kuona yeye aliyeninunua kwake.

 

4. Ulimwenguni humu, matata na kuchoka. Nikihitaji kitu nafadhahika bure, lakini siku ile kuu nita’pomwona Mwokozi, natumaini sitakosa dhawabu yangu!

 

5. Mbinguni sitaona adui zangu tena. Hayatakuwa mambo yakupokonya pale. Sauti nitamtolea, kusema: Mungu, haleluya! Mikono nitaipepea kwa shangwe kuu!


Video imeimbiwa na METHUSELA Bushambale na DAVID IMANI

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=IyxLpC7tyaw?feature=oembed&w=500&h=281]

THAMBI