Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

273. NI uheri kumwamini Mungu

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

273

1. Ni uheri kumwamini Mungu kama Ibrahimu wa zamani. Hakutiwa shaka kwa uchungu, ila alitii kwa imani. Ni uheri kuendea sawa katika mapito ya sheria. Ukijaribiwa na kukawa, mwisho Mungu atakujalia.

 

2. Mashujaa wote wa Biblia hawakufurahia anasa. Wakafunzwa kutumainia Mungu na uweza wake hasa. Tena wakaenda kwa imani ya kutetemesha ulimwengu, wakashinda giza na shetani. Sifa na heshima zina Mungu!

 

3. Yesu atakaye kuzwa naye kwanza adhiliwe kuwa vumbi; Mwana wake mwema na ambaye baba humpenda, humrudi. Hivyo Mungu awakamilisha watu wake kwa mateso huku, na zaidi kuwafahamisha kulijua pendo lake kuu.

 

4.Na ikiwa raha ya dunia yatoweka katika jaribu, mwaminifu atafurahia Mungu wake, kwani yu karibu. Na mavuno ya taabu yake yakichomwa na kuharibika, atategemea Bwana wake na kwa hiyo hata nung’unika.

 

5.Jipe moyo, enyi kundi dogo, na msiogope hatarini! Shika neno la Mwenyezi Mungu, litawaongoza safarini! Haleluya, kwani majaribu yahimiza msafiri mwendo, hata ataona kwa karibu mji wa amani na upendo!

Emil Gustavsson, 1889

No comments yet.

Leave a Comment