272. NANI ni wa Yesu

271

1. Nani ni wa Yesu? Amtumikie! Atafute watu na kuwahubiri! Nani anataka kujitoa leo, kufuata Yesu katika mateso?

Pambio
Nani ni wa Yesu? Amtumikie! Nani atakaye na amwitikie! Mimi ni wa Yesu, nimtumikie, nitafute watu, kwake warudie!

 

2. Kwa upendo wake tunalazimishwa kutafuta wenye dhambi na makosa. Tunaendelea kuwavuta kwake, hata wanaomba: Mungu tuokoe!

 

3. Yesu alitununua sisi sote ju’ ya msalaba na kwa damu yake. Kwake tumepata raha na uhuru; tunataka sasa kuwa waaminifu!

 

4. Hata vita ikiongezeka huku tunayo bendera ya kushinda kwetu. Siku ya hatima inakaribia, itaibadili vita iwe shangwe.

Frances R. Hauergal