266. AYALA naye anayo shauku

 266

1. Ayala naye anayo shauku ya maji ya kisima; na vivyo hivyo ninaona kiu kwa Mungu wa uzima.

Pambio:
Kama ayala aonavyo shauku mito ya maji safi, na vivyo hivyo rohoni mwangu naona kiu kwa Mungu wangu.

 

2. E’ Mungu wangu, Mungu wa fadhili, nakutafuta wewe! Je, nikuone lini kwa ‘kamili, niburudishwe nawe!

 

3. Nazifikiri siku za zamani niliposhangilia. Nijaze tena raha na amani, nakutumainia!

 

4. Na usifadhaike moyo wangu, amini Mungu wako! Fadhili zake hata huko mbingu zatosha sana kwako!

H.E. Lute