263. ENYI kundi lake Mungu

263

1. Enyi kundi lake Mungu, muda haba mhimili! Kati’ nchi ya milele mtaona raha tele.
:/: Muda haba, muda haba, tena vita itakwisha. :/:

 

2.Usilogwe na dunia, usiache Mungu wako! Katika mabaya, mema ufuate Bwana Yesu.
:/: Siku zote, siku zote! Hivyo utashinda vyote. :/:

 

3.Ukichoka safarini, ukiona njia ndefu na hatari za jangwani, Mungu akuburudisha.
:/: Raha huko, raha huko yatuliza msafiri. :/:

 

4. Kwa imani tunaona nchi yetu ya ahadi. Ni habari nzuri sana: Majaribu yatakoma.
:/: Mbio sana, mbio sana huko ju’ tutaonana. :/:

 

5. Tukiitwa na mauti kwa furaha tutahama. Tulivyovitumaini, ng’ambo huko tutaona.
:/: Heri tele, heri tele: ‘ona raha ya milele! :/: