260. MWENYEZI amejenga mji

260

1. Mwenyezi amejenga mji, Mfalme wa huko ni Yesu, Yohana aliouona kushuka kutoka mbinguni. Ukuta ukawa wa jaspi, na njia ya dhahabu safi. Wakati nitakapohama, nitachukuliwa Sayuni.

Pambio:
Mjini mle mtakatifu Yesu atuandalia makao. Sasa nangoja, nautamani mji mzuri kutoka mbinguni.

 

2.Na dhambi hazitafikapo, uchafu hautaingia, mateso, ugonjwa na kufa hazitakuwapo mjini. Na mle tutayasahau mashaka, ‘jaribu na vita; hatutaachana milele. Hakuna uchungu rohoni!

 

3. Mjini hatutayaona kilio na maombolezo. Na huko hatutadanganywa, haitakuwamu husuda. Na wana wa Mungu waona uzuri na utakatifu; nitakapofika mjini nitashangilia daima

 

4. Wapenzi, rafiki na wale waliomaliza safari, watashangilia kabisa kwa’jili ya damu ya Yesu. Na tutawaona mjini katika makao ya raha. Tumaini letu ni hili: Tutakusanyika mbinuni.

 

 

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=sVng7N4UtRc?feature=oembed&w=500&h=281]