259. NAFIKIRI siku tutakayofika huko kwetu

259

1. Nafikiri siku tutakayofika mbinguni huko kwetu, na malaika kwa furaha watatukaribisha.

Pambio:
Wataimba wimbo wakutupokea: “Karibuni! Karibuni wote kwetu!” Malaika wa Mungu watatulaki kwa nyimbo za furaha: “Twawasalimu! Karibu kwetu!”

 

2. Mkutano ‘kubwa umekwenda mbele na sasa uko kule. Huimba kwa sauti kuu ukimsifu Mungu.

 

3. Sisi nasi tutakusanyika huko Yerusalemu mpya, na mkutano wa wakristo utatuamkia.

 

4. Bwana Yesu naye atatupokea, atatukumbatia katika nyumba ya mbinguni iliyo ya milele.

Fredrik Engelte