257. SIKU ya kuisikia parapanda

257

1. Siku ya kuisikia parapanda yake Mungu, ikiita wateule wake wote, kwa neema tutakaribishwa na Mwokozi wetu katika kutano kubwa huko juu.

Pambio:
Tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake katika kutano kubwa huko juu.

 

2. Mungu anawafufua wafu wake siku ile, na wakristo hai watabadilika, wote watanyakuliwa kumkuta Bwana Yesu, tutakusanyika wote huko juu!

 

3. Wimbo wa mbinguni kama maji utakapovuma, utukufu wake Yesu tuta’ona. Nami pia kwa neema nitafika siku ile kusikia neno lake la “karibu!”

James M. Black, 1893
When the trumpet of the Lord shall sound, R.S. 528