256 ASUBUHI na mapema

256

1. Asubuhi na mapema siku ya habari njema twende sote Bethlehemu! Mungu ameturehemu!

 

2.Nyota kubwa inang’aa ju’ ya nyumba ana’kaa Mwana wake wa pekee. Mbele yake tujiweke!

 

3. Wachungaji wasikia nyimbo zao malaika: ” Asifiwe Mungu juu, duniani raha kuu!”

 

4. Mariamu anachoka, safarini wana’toka, analaza mwana ndani ya sanduku la majani.

 

5. Wachungaji wanafika, na magoti wana’piga; waliacha kundi lote kushukuru Yesu wote.

 

6. Mwana yule ni Mwokozi, msaada, Mkombozi. Neno la kuaminiwa, Mungu ametushukia!