255 ZIMETIMIZWA Ahadi njema

255

1. Zimetimizwa ahadi njema: Amezaliwa Mwokozi wetu! Na yote Mungu aliyosema kwa manabii kwa ajili yetu, tumeyapata na kuyaona katika Yesu, mwanawe Mungu. Alitujia na tumepona, twaweza wote kufika mbingu.

 

2. Alijidhili kuwa maskini, na alifika ulimwenguni, Mwokozi wetu, twaiamini. Walimlaza katika hori. Na utukufu kwa Baba yake aliuacha, rehema kuu! Na twende sote horini kwake, tumsujudu aliye juu!

 

3. Mtoto huyo – mfano wetu, si mtu tu, bali Mungu pia. Akawa mwenye kutukomboa, kwa Golgotha alitufilia. Tulipotea vibaya sana katika dhambi na ukaidi, kwa umaskini wa Yesu Bwana twapata kuwa wote tajiri.