252 NINAKUSHUKURU Mungu kwa fadhili

252

1. Ninakushukuru Mungu kwa fadhili zako zote, kwa furaha na uchungu, kwa neema njia yote! Kwa kipupwe na masika, kwa wakati wa machozi. Na kwa raha kadhalika na’shukuru Mkombozi!

 

2. Ninakushukuru Bwana kwa kunifunua siri, kwa kusikiliza sana, ombi na kulifikiri! Na kwa msaada wako, kwa wakati wa jaribu. Kwa agano la Mwanako nashukuru! U karibu.

 

3. Nashukuru wewe pia kwa uzuri wa mbinguni, nuru ulioitia, na kwa jambo la huzuni! Kwa jaribu na kwa giza na kwa siri ya imani, tena kwa kunijaliza ninakuwa na shukrani!

 

4. Kwa waridi za njiani na miiba yao pia, kwa mahali pa amani uliopotuandalia, kwa agano la upendo, kwa kutupa tumaini, kwa kifiko cha mwenendo: Nashukuru! U amini!

Augut Storm, 1891

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=4Z8qtBi6IDY?feature=oembed&w=500&h=281]