250 IKAWA siku kubwa kwangu aliponiokoa Yesu

 250

1. Ikawa siku kubwa kwangu aliponiokoa Yesu. E’ roho yangu umsifu Mwokozi wako Yesu Kristo!

Pambio:
Siku kuu, siku kuu aliponiokoa Yesu! Na kwa neema na upendo akaondoa dhambi zangu! Siku kuu, siku kuu aliponiokoa Yesu!  

 

2.Nimeokoka, nafurahi! Ananitaja mwana wake! Alinivuta kwa upendo, nikafuata mwito wake.

 

3.Ni shangwe ku’ moyoni mwangu nikifuata Bwana Yesu. Anipimia ne’ma sawa wakati wote ma maisha.

 

4. Kwa pendo kubwa na rehema ananitunza siku zote. Sitasaahu siku ile aliyoniokoa Yesu.

Oh, happy day, R.Sl 622; R.H. 619