249 ZAMANI mjini mwa Yerusalemu

249

1. Zamani mjini mwa Yerusalemu waisrael’ waliabudu. Wakristo wa sasa wanakusanyika kuomba, kusifu Mwokozi.

Pambio:
Msifuni, msifuni Mungu wetu, kwani ametutendea mema! Tutamsifu tu aliyetoka ju’, shangilieni Mwokozi mwema!

 

2. Mwokozi yu nasi, ame’fumbulia uweza wa kutuokoa. Na yu mwaminifu, atusikiliza, apenda kutupa baraka.

 

3. Twaomba baraka na mvua ya mbingu kuithibitisha Injili! Wagonjwa wapone, vipofu waone, Tupate ‘batizo wa Roho!