247 NAPENDA sana kumushukuru Mwokozi

247

1. Napenda sana kumshukuru Mwokozi wangu kwa nia huru; kwa wimbo wangu nashuhudia upedo wake na damu pia.

 

2. Nikishukuru mateso yake msalabani na kufa kwake, nataka katika wimbo wangu kumtolea shukrani yangu.

 

3. Naimba sasa, nina faraja, katika Yesu nina faraja. Ni mambo tunayofunuliwa, kwa wenye dhambi yamefichwa.

 

4. Kwa neno lake ananiambia kwamba ananihurumia, na ukombozi ninao sasa kwa damu iliyonitakasa.

 

5. Na msione ajabu sana ya kuwa namshukuru Bwana! Ninamwimbia kidogo sasa, ‘taendelea mbinguni hasa.

 

6. Anipa vyote kwa pendo lake, urithi wangu wachungwa kwake hata wakati wakuhamia mbinguni, na nitashangilia.

Anders Nilsoon