244 SAFARI yangu huku ikiwa hatarini

244

1. Safari yangu huku ikiwa hatarini, na ikipita katika giza na jaribu, najua kwa hakika: Mwokozi yu karibu, ninamfuata mahali po pote.

Pambio:
Nikiwa pamoja na Yesu sina hofu. Anipa furaha na heri rohoni mahali pote. Ikiwa nitayashiriki mateso yake, nitamfuata Mwokozi hata mwisho.  

 

2. Nikitangaza neno la Mungu duniani katika mataifa walio wakaidi. Nina furaha kubwa moyoni mwangu, kwani Mwokozi yu nami mahali po pote.

 

3. Na Bwana akitaka nibaki hapa kwangu, wengine wakitumwa mahali pa ugeni, kusudi langu moja: nidumu mwaminifu, na nimfuate mahali po pote!

 

4. Si lazima nijue makusudio yote, ni kazi yangu huku kumfuate yeye. Ikiwa nitabaki, ikiwa nitakwenda, nitamfuata Mwokozi po pote.

C. Austin Miller
It may be in the valley, R.H. 465