242 MAISHA yangu yote nimali ya Mwokozi

242

1. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Maungo, roho na akili, yeye ameyabadili. Siku zangu zote ni mali ya Mwokozi.

Pambio
Wakati wangu wote ni mali ya Mwokozi. Machoni pake ni amani, natumika kwa shukrani. Namsifu Yesu, amenihurumia!

 

2. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Naomba niwe mpendevu, nitafute wapotevu! Aliwanunua kwa damu takatifu.

 

3. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Unijalie kati’ mwendo kuongoza kwa upendo wana wapotevu, wapate kuokoka.

 

4. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Nakaa miguuni pake, siku moja huko kwake inapita elfu pengine bila Yesu!

W.C. Martin