237 MWOKOZI wangu ni mwamba bora

237

1. Mwokozi wangu ni mwamba bora, ahadi kama milima; zaniletea amani tele, na mibaraka daima. Katika mwamba ni raha kuu, baraka tele kutoka juu. Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele.

 

2. Makimbilio ni mwamba huo katika teso lo lote; Nisikimbie adui ‘kuu, nishinde katika vyote! Dunia yote ikitingika, ahadi zake hazipunguki. Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele.

 

3. Nakaa mbali ya udhalimu, hatia, dhambi, hukumu. Na kwa imani nikisimama, adui atakimbia. Nayo mawazo ya giza tupu hayatapata nafasi huko. Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele.

 

4. Nafurahia baraka zote za ulimwengu wa roho. Karama hizo nalizipewa katika kufa kwa Yesu. Hakuna woga na shaka huko, hayatakuwa manung’uniko. Nakaa humo, ninastarehe, ni heri sana milele.

Otto Witt