236 DHAIFU mwenye dhambi

236

1. Dhaifu, mwenye dhambi, nilipotea njia, lakini Bwana Yesu alinihurumia. Nategemea yeye, najua pendo lake, ajaza roho yangu, ninavyo vyote mwake.

Pamio:
Ajaza roho yangu, apita vitu vyote. Amani na upendo ni zangu siku zote. Ajaza roho yangu, neema kubwa kwangu! Namhimidi Yesu: Yu yote ndani yangu.

 

2. Sitaki dhambi tena, haiku’faidia; rafiki yangu, Yesu, ananisaidia. Alitangua dhambi kwa msalaba wake, kwa yeye ukombozi, na vyote vimo mwake.

 

3. Napenda kufuata daima nyayo zake, nibadilishwe sana, nifananishwe naye! Na tena siku moja atanikaribisha nyumbani mwake Baba, na atanijaliza!

Otto Witt