Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

234 UTUKUFU wa mbinguni niwa heri na amani

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

234

1. Utukufu wa mbinguni ni wa heri na amani, dhambi hazitakuwamo. Vitu vyote vilivyomo ni vya tunu na thamani, dhambi hazitakuwamo.

Pambio
Dhambi hazitaingia mbingu ya utakatifu. Ukidumu mwenye dhambi bila kutakaswa huku, hutaingia mbinguni.

 

2. Kama unatumaini kufikia nchi ile na kuona Bwana Yesu, utafute utakaso na kupata moyo safi! Dhambi hazitakuwamo.

 

3. Unaweza ‘tenda dhambi na kukana Bwana Yesu, walakini ukumbuke: Dhambi zako zitafunga lango la mbinguni, kwani dhambi hazitakuwamo.

 

4. Na ukiwa mkaidi hata sa’ ya kufa kwako, utaitwa hukumuni, na utaambiwa huko: “Ondokeni siwajui!” Dhambi hazitakuwamo.

Pambio:
Ukitaka kufikako mbingu ya utakatifu, tubu sasa, hacha dhambi, utafute moyo safi, na utaingia mbingu!

C.W. Naylor

No comments yet.

Leave a Comment