232 NILIPOFIKA kwa bwana Yesu

 232

1. Nilipofika kwa Bwana Yesu, nikapaaza sauti yangu: “Yesu Mwokozi, unirehemu!” Akaniokoa.

:/: Yesu asifiwe! :/: Alisikia kilio changu, Yesu asifiwe!

 

2. Nilipofika kwa Bwana Yesu, nikamsihi Mwokozi wangu: “Unitakase, nifanye safi!” Akanisikia.

:/: Yesu asifiwe.:/: Alisikia maombi yangu, Yesu asifiwe!

 

3. Ona kisima cha msalaba, leo kingali chabubujika kuniokoa na kusafisha! Yesu asifiwe!

:/: Yesu asifiwe:/: Aniokoa, anisafisha, Yesu asifiwe!

 

4. Njoo kwa Yesu, kisima hicho, unywe, uoshwe katika maji! Kiu yapoa, na watakaswa, Yesu asifiwe.

:/: Yesu asifiwe! :/: Kiu yapoa, na watakaswa, Yesu asifiwe!

E.A. Hoffman, 1877
Down at the Cross, R.S. 192