Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

231 MWOKOZI alitoa damu kwa’ jili ya waovu

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

231

1. Mwokozi alitoa damu kwa’jili ya waovu, msalabani alikufa kuniokoa mimi.

Pambio
E’ Yesu, niokoe sana, nifunze kuamini! Na unilinde tena, Bwana, nisipotee kamwe!

 

2. Alijitwika dhambi zetu, huzuni na maradhi; neema kubwa, wema wingi, upendo wa ajabu!

 

3. Na hapo jua likafichwa, ikawa giza kuu; muumba alitufilia kutulipia deni.

 

4. Magoti yangu nayapiga msalabani pake, na kwa machozi natazama mateso yake huko.

 

5. Nitakurudishia nini, Mwokozi wangu mwema? E’ Bwana, nikutumikie maisha yangu yote!

Isaac Watts
O Lord, remember me

No comments yet.

Leave a Comment