229 MWOKOZI Mfalme, ulisulubiwa

229

1. Mwokozu Mfalme, ulisulibiwa, e’pasaka wetu, ulidhihakiwa. Ukatoka damu, ‘kaona uchungu ulipotimiza mapenzi ya Mungu. Huku Gethsemane ulihuzunika, kwa neno la mbingu ukafarijika. Katika kuomba ukatiwa nguvu, na mwisho ukafa tupate wokovu.

 

2. Kwa ‘jili ya mimi ulijeruhiwa, ukaonja kufa, nipate uzima. Ulijisahau, ukanikumbuka, uliwaombea waliokutesa. Na ulijitoa dhabihu ya kweli, na kuusikia uchungu mkali. Kwa pendo kamili ulikusudia kuonja mauti kwa ‘jili ya wote.

3. Je, kupatanishwa na Mungu ni nini? Ni kwamba laana la dhambi lakoma. Kufika karibu na Mungu ni nini? Ni kuwa rafiki wa Mungu wa mbingu. Na sasa ufike kutoka dhambini, utie hatia na dhambi nuruni! Mwokozi mpendwa akuhurumia, atakufungua na ‘kusaidia.

Fr. E. Falk