228 WAKATI wa utoto wako

228

1. Wakati wa utoto wako, hujapoona shida bado, sauti ilikuambia: “Unipe sasa moyo wako!”

Pambio:
Wajua ni nani huyu anayekuita sasa? Ni Yesu, rafiki yako; anakuita: ” Njoo kwangu!”

 

2. Na katika ujana wako wausikia mwito wake, na jinsi utakavyoshinda shetani akikujaribu.

 

3. Wakati wa uzee wako dhambini ukiendelea hata kukaribia kufa, Mwokozi akuita tena.