223 NI UHERI bora kumwamini

 223

1. Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu kwa wakati wa ujana wetu, kabla hatujazionja dhambi na mashaka zinazoharibu roho zetu.

Pambio:
Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu, na kumfuata kila siku. Na ujana wetu ukitukimbia tena, shangwe ya wokovu itabaki.

 

2.Ni uheri bora kumtii Bwana Yesu kwa wakati wa ujana wetu. Hivyo tutakuwa na dhamiri safi, njema kwa maisha yetu yote pia.

 

3.Ni uheri bora kumtumikia Yesu kwa wakati wa ujana wetu. Bwana Yesu akumbuka kila tendo dogo, atalipa kwa neema yake.

 

4.Ni uheri bora kumngoja Bwana Yesu kwa wakati wa ujana wetu. Atatuchukua kwake kwa furaha kubwa, tutakuwa naye siku zote.