222 BWANA Yesu amesema

1.Bwana Yesu anasema: “Dhaifu wewe sana. Mimi ni mchunga mwema”. Na kwa hiyo namwandama.

Pambio: Yesu alikufa kwa ajili yangu, aliziondoa dhambi, furaha kubwa kwangu!

2.Pendo la Mwokozi wangu limeyeyusha moyo. Ametoa dhambi zangu na kiburi na uchoyo.

3.Sina kitu mkononi cha kunifaidia; udhaifu u moyoni, Yesu ninamlilia.

4.Mungu akisaidia nitamaliza mwendo. “Yesu alinifilia”, nitaimba huko ng’ambo.

5. Siku moja nitafika mbinguni huko juu, nitaimba kadhalika shukrani kuu.

Elvina M. Hall- T.Truvé
Min Jesus säger mig, Sgt. 419; I hear the Saviour, R.H. 198