219 HATUMUJUI rafiki mwema

 219

1. Hatumjui rafiki mwema, ila Yesu, ila Yesu; yeye mwenyewe atufahamu, yeye Bwana peke yake.

Pambio:
Yesu anatujua, pia Yesu anatuonya njia. Yesu rafiki kupita wote, wote, wote pia wa dunia.

 

2. Hatumjui rafiki mwema kama Yesu, Bwana Yesu. Na pendo lake ni la ajabu, linadumu siku zote.

 

3. Je, ataweza kutusahau? Hataweza ku’sahau. Twafarijiwa kwa pendo lake kila siku, kila siku.

 

4. Nani ashika agano lake? Bwana Yesu peke yake. Alikataa kusaidia? Hataweza kukataa.

 

5. Nani rafiki mpendwa wangu? Bwana Yesu peke yake. Anastahili kupata sifa huku chini na mbinguni.

Johnson-Oatman
There’s not a friend, RH. 110