212 SAUTI ya Yesu niliisikia

212

1. Sauti ya Yesu niliisikia, kwa pendo aliniambia: “Ufike, nataka kukusaidia, nangoja, nangoja, ufike!”

Pambio:
Njoo kwa Yesu, ufike upesi, uupokee wokofu wa Mungu! Mbona kukawa dhambini, rafiki? Yesu anakuita, njoo!

 

2. Ukiwa na hofu kufika kwa Yesu, uliye na dhambi rohoni, kumbuka ya kuwa huruma ni tele; ufike kwa Yesu, angoja!

 

3.Ukiwa maskini, dhaifu kabisa, Mwokozi anakufahamu. Anakuambia: ” Pokea neema, uache mzigo wa dhambi!”

 

4. Na kama nilivyo ninamfikia Mwokozi aliyenipenda. Ninaupokea wokovu na raha; kwa shangwe ninamshukuru!