209 UWATAFUTE wanao potea

209

1. Uwatafute wanaopotea, na kwa upendo watoe dhambi! Lia pamoja na wenye huzuni, uwapeleke kwa Yesu Mwokozi! Uwatafute wanaopotea! Yesu Mwokozi awahurumia.

 

2. Anatafuta waliokimbia, anawangoja warudi upesi. Uwafundishe kwa pendo na kweli ju’ ya neema na haki ya Yesu!

 

3.Ndani ya roho na katika siri labda waona shauku ya Mungu. Uwaongoze kwa Yesu Mwokozi, wafahamishe upendo wa Mungu!

 

4.Uwatafute wanaopotea! Mungu atoa upendo na nguvu. Uwapeleke kwa Yesu mpozi, Mwenye huruma na afya kwa wote!

Fanny Crosby, 1869
Rescue the perishing, R.S. 345; R.H. 561