Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

207 UMGEUKIE Mwokozi

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

207

1.Umgeukie Mwokozi, jitenge na ovu na dhambi! Babako angoja ufike; usiangamie milele!

 

2. Kijana, unafurahia maisha na mambo ya nchi. Baada ya muda kitambo utahukumiwa na Mungu.

 

3. Kwa nini kujiangamiza katika tamaa za huku? Usijipoteze dhambini! Dunia isikuharibu!

 

4.Umkimbilie Mwokozi, atakupokea kwa pendo, na utaokoka hakika kwa nguvu ya damu ya Yesu!

 

5. Walio mbinguni waimba, wanayo mavazi meupe; hutaki sehemu pamoja na wao nyumbani mwa Baba?

 

6. Je, mwisho utaona wapi mahali pa kujisitiri? Dunia itakapochomwa utakosa makimbilio.

 

7. Ujipatanishe na Mungu, na usichelewe, rafiki! Ukimkataa Mwokozi, utatupwa nje gizani.

 

8. Chagua pasipo kukawa! Mwokozi atakupokea. Angoja ufike kutubu; atakutakasa kwa damu.

No comments yet.

Leave a Comment