206 RAFIKI yangu tazama

206

1. Rafiki yangu, tazama, wapita njia ya wapi? Milele, je? utakaa wapi ukikataa Mungu?

Pambio:
Ujiandae sasa, utakutana na Mungu! Lazima uwe tayari
kwa sababu utamuona!

 

2.Dunia haina raha, amani wala salama. Fahari yake ikikuloga, utapotea njia.

 

3. Lo! Yesu anakuita! Kwa nini unachelewa? Ushike njia ufike kwake! Ataja jina lako.

 

4.Uache haya na hofu, Mwokozi anakupenda! Kwa damu alikomboa wewe, anakutaka sasa.

 

5.Ikiwa unachelewa kupatanishwa na Mungu, utamkuta Mwokozi kama mwamuzi mwenye haki.

Oscar Hallof, 1921