203 HATUA moja kati ya wewe na Mwokozi

203

1.Hatua moja kati ya wewe na Mwokozi. Wakawilia nini? Ufike kwake leo!

Pambio:
Hatua moja, hatua moja, njoo akungoja! Njoo kutubu dhambi, atasamehe zote! Usikatae tena wokovu wake Mungu!

 

2.Hatua moja mbele, anakungoja sasa. Amini neno lake, na utapata raha!

 

3.Hatua moja mbele, uzima uta’ona. Siku si nyingi huku, ‘jitoe kwake Mungu!

 

4.Hatua moja mbele, kwa nini kukawia? Omba: E’ Bwana Yesu, unipokee sasa!

Fanny J. Crosby