Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

215 MWENYEZI Mungu anafanya ishara kubwa Duniani

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

215

1. Mwenyezi Mungu anafanya ishara kubwa duniani, anaondoa minyororo inayofunga watu huku. Avunja nyavu za shetani, na wakosaji waokoka.

 

2. Maneno yake yana nguvu kushinda yote ya zamani. Na watu wanapiga mbio kuomba ne’ma ya Mwokozi. Wakiyapata masamaha, waimba wote: “Sifu Mungu!”

 

3. Tazama, ndugu wengi sana wanafuata Yesu leo; katika kila nchi sasa maelfu wanapenda Mungu. Wengine wanavutwa naye Mwenyezi Mungu, Baba yetu.

 

4.Inua macho, mvunaji, mavuno yanaiva sana! Uende kutafuta watu, uwapeleke kwake Yesu! E’ ndugu wote, amkeni, ‘kawaokowe wenye dhambi!

 

5. Wengine wanapoingia ufalme wako, Yesu Kristo, nisibakie huku chini, neema hiyo nakuomba! Nakaa mikononi mwako, unifikishe huko kwako!

 

6.Najua siku ni karibu Mwokozi atakaporudi, awachukue watu wake mpaka nchi ya amani. E’ siku ya uheri bora, nakutamani. Uje mbio.

Nils Frykman, 1877

No comments yet.

Leave a Comment