20 BWANA Yesu uniongoze baharini huku chini

20

1. BWANA Yesu, uniongoze Baharini huku chini, Juu ya mawimbi mengi, Katika dhoruba kali! Bwana Yesu, uniongoze, Nakutegemea wewe.

2. Bwana Yesu, uniongoze, Utulize moyo wangu! Neno moja kwako, Marashwari baharini. Bwana Yesu uniongoze, Nipe utulivu wako!

3. Bwana Yesu uniongoze, Niyashinde majaribu! Mengi ya kunidanganya, Mengi ya kufunga macho! Bwana Yesu uniongoze, Niwe mshinadji kweli.

4. Bwana Yesu uniongoze, Siku nita’vuka ng’ambo! Nikiona woga , giza, Nipe nuru na amani! Bwana Yesu, uniongoze, Uwe nami hata mwisho!