199 NJONI wote muteswao

 199

1. Njoni wote mteswao! Wote wenye sikitiko kwa ajili ya makosa, mje sasa kwa Mwokozi! Kwake mtaona raha, utulivu na amani. Matulizo mioyoni mtapata kwake Yesu.

 

2.Hataacha sikitiko kulemea moyo wako; Yesu ni mchunga mwema, akuficha mazizini. Pendo lake lina nguvu, huchukua masumbuko, hufariji roho yako, hukutwaa kwake Mungu.

 

3. Yesu kama nyota nzuri ing’aayo asubuhi, mtu amfuataye ataona njia wazi. hata nyota za mbinguni zikiteketea zote, nyota hiyo ya milele haitazimika kamwe.

 

Tune: Who can cheer the heart like Jesus, R.H. 518; MA. 490