197 HAPO nilipokua dhambini

197

1. Hapo nilipokuwa dhambini, niliumwa kwatika roho. Sasa ninafurahi kwa shangwe kwani Yesu ameniponya.

Pambio:
Ndiyo kazi kubwa ya ajabu: Mwokozi aliniokoa! Naye anapenda watu wote, atakuokoa wewe.

 

2. Dhambi zote nilizozitenda zimefutwa na Bwana Yesu. Sikitiko kwa ‘jili ya dhambi zilikoma nilipotubu.

 

3. Sasa mimi sitaki kurudi, nachukia kabisa dhambi. Nimeonja furaha ya Mungu na amani na raha yake.

T. Allan Törnberg