Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

196 USIEIFANYA bidii kabisa

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

196

1. Usiyefanya bidii kabisa, hutaingia mbinguni. Uikinge roho kwa neno la Mungu, usipotee milele! Njia ni nyembamba na mlango ‘dogo, ujitahidishe kuingia humo! Ukubali leo wokovu wa Mungu ili ufike mbinguni!

 

2. Vizuio vingi katika safari, mwovu anakujaribu. Uvishinde vyote vinavyozuia, vyote katika dunia! Usimfuate kila aitaye, ungeweza kupoteza roho yako! Bwana Yesu anakupenda daima; ujitahidi kabisa!

 

3. Pasipo imani huwezi kufika hata bandari salama wala kuingia katika uzima; hilo ni neno la Mungu. Kwa imani tupu utaokolewa, usikie sasa neno la wokovu! Tubu dhambi zako, amini Mwokozi; hiyo ni njia, hakika.

 

4. Mungu anaita, wo wote wafike, waupokee uzima! Atakupa nawe hazina ya mbingu, ukitafuta kwa kweli. Mungu Baba anapenda roho yako, Yesu anataka kuokoa wewe, Roho ‘takatifu anakuamsha.

 

Ukiitika u heri! T. Lars Linderot, 1798

No comments yet.

Leave a Comment