Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

193 NINENO zuri la ‘aminiwa

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

193

1. Ni neno zuri la ‘aminiwa, listahililo kukubaliwa, ya kwamba Yesu alitujia awaokoe wenye makosa.

 

2. Wa kwanza mimi wa wenye dhambi, lakini ninafurahi sasa sababu Yesu, Mwokozi wangu, aliniosha kwa damu yake.

 

3. Mwokozi wetu yu nasi hapa, atenda kazi kwa nia yake; awasha moto rohoni mwetu, uwezo gani utampinga?

 

4. Viziwi wanasikia sasa, viwete wanatembea sawa, wenye ukoma watakasika, Injili yake yahubiriwa.

 

5. E’ Bwana Yesu, tupulizie, tujaze Roho Mtakatifu! Uwaamshe waliokufa katika dhambi, uwaangaze!

 

6. Fungua mbingu unyeshe mvua panapo kiu na jangwa tupu! Uligeuze, likachanue na kufurahi kwa shangwe kuu!

 

7. Na mataifa wakusujudu mahali pako patakatifu! Amina. Wako ni utukufu na sifa zote! Haleluya!

Joel Blomkvist, 1876

No comments yet.

Leave a Comment