192
1. Sauti moja iliniuliza: ” Wajua nilikufanyia nini? :/: Kwa’jili yako niliteswa sana; ufike kwangu, kwani nakupenda! ” :/:
2. ” Nilipokuwa huku duniani wakanitia taji ya miiba, :/: Na sikupambwa fedha na dhahabu, lakini majeraha na uchungu.” :/:
3. ” Golgotha nilifika siku moja, na nilikufa ju’ ya msalaba. :/: Tazama, katika mikono yangu nimekuchora, e’ mtoto wangu.”:/:
4.Heleluya, rohoni ninaimba! Nimejiweka mikononi mwake. :/: Na Yesu ananiongoza sasa, nifike nchi nzuri huko juu. :/:
K.E. Svedlung