191 YAPIGWA hodi kwangu

191

1. Yapigwa hodi kwangu, mgeni a’fika, akiniomba: “Nifungulie! Umande umeshuka kichwani usiku, na nywele zangu zimelowa maji”.

 

2. A! Huyu si mgeni, ni Yesu Mwokozi, sauti yake nzuri na’jua. Ninamfungulia, naona ni Yesu; na siku hiyo sitaisahau.

 

3. Anong’oneza sasa rohoni: “U wangu”, karibu naye ninatulia. Ananitia nguvu, baraka ya mbingu; daima nitakaa kwake Yesu.

 

4. Ni kweli, mimi ni wa Mwokozi milele, amenitaja: “Ndugu, mpenzi”. Ananikarimia hazina za mbingu, ninaingoja siku ya arusi.

Fr. Schibboleth. arr L.P