19 MUNGU tunangoja wote Roho yako ‘Takatifu

19

1. MUNGU tunangoja wote Roho yako ‘takatifu, Tunaomba kwa imani “Umtume hapa kwetu!

 Refrain : Mungu wetu, Mungu wetu, Umimine Roho yako, mioyoni mwetu, Bwana utimize kazi yako!

 

2. Washa moto wako tena, ndani ya mioyo yetu, Hata vyote vya majani vitateketea sana!

 

3. Utakase roho zetu, Na kiburi uivunje! Wewe U mfalme wetu, utawale watu wako!

 

4. Utujaze siku zote Pendo lako kubwa, Mungu! Sisi tuwe nyumba yake, Roho yako takatifu!

 

5. Na karama zake Roho utuzigawie Bwana! Na wangonjwa uwaponye, Wote wakuone Mungu!