189 UNIHUBIRI habari njema

189

1.Unihubiri habari njema, neno la ukombozi, hata ikiwa siufahamu wingi wa wema! Nilipokuwa katika giza, ndipo Mwokozi alinijia, na akanipa wokovu, raha na tumaini.

Pambio:
Mimi kipofu, naona sasa, anasikia maombi yangu, naye hatanisahau, kwani ananipenda.

 

2. Amefungua mkono wake, kuna wokovu humo; ukilemewa moyoni mwako, uje kwake Yesu! Uliyechoka kwa dhambi zako, umtazame Mwokozi wako, na utapata wokovu, njoo, anakupenda.