184 NITAKWENDA mahali pa giza

184

1. Nitakwenda mahali pa giza na dhambi kuhubiri Injili ya nuru, ili watu wasiosikia habari wafahamu upendo wa Yesu.

Pambio:
Nitakwenda mahali pa giza na dhambi, hata wote wapate kuona wokovu.

 

2. Akitaka niende kwa watu wagumu na kuacha rafiki na ndugu, hata wakinitaja: ” ‘pumbavu ” na “bure”, nachagua mapenzi ya Yesu.

 

3.Uliyezipoteza dakika na saa kwa tamaa ya mambo ya huku, uamke na uwaokoe wenzako, hata wasipotee kwa dhambi!

 

4. Watu wengi wangali watumwa gizani, wanangoja kupata uhuru, Yesu ananituma, niende upesi kuhubiri maneno ya nuru.

Margeret M. Simpson