179 SIKU moja mavuno yataisha kabisa

179

1. Siku moja mavuno yataisha kabisa, baada ya hayo hukumu.
Jua litazimika siku hiyo ya mwisho, na hutasikia injili

Refrain:
Atakusanya ngano kwa furaha ghalani bali makapi yote yatatupwa motoni rafiki utakuwa wapi

2. Mahubiri na nyimbo za wokovu wa mungu zitakaponyamaza huku,
uliyelikataa neno zuri la mungu, utakaa wapi milele

Refrain:
Atakusanya ngano kwa furaha ghalani bali makapi yote yatatupwa motoni rafiki utakuwa wapi

3. Watu wote wa mungu wafikapo mbinguni kukaa pamoja na yesu,
wataimba kabisa kwa sauti nguvu kumshangilia mwokozi

Refrain:
Atakusanya ngano kwa furaha ghalani bali makapi yote yatatupwa motoni rafiki utakuwa wapi


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=O7D8fB3IyJs?feature=oembed&w=500&h=281]