175 SHAMBA la Mungu limeiva

175

1. Shamba la Mungu limeiva, litayari sasa kuvunwa. Wavunaji mfike mbio kuyavuna mavuno yake!

Pambio:
Bwana Yesu, twakuomba, uwatume watenda kazi wakusanye miganda yote kwako Yesu, Mwokozi mwema!

 

2.Uwatume mapema sana, na wengine kati’ mchana, hata saa ya magharibi uwaite wavuni wako!

 

3. E’mkristo anakuita, wende mbio, usichelewe! Macho yako uyainue kwani Yesu aja upesi!

J.O. Thompson, 1894