172 SISI tu viungo vya mwili’ moja

172

1. Sisi tu viungo vya mwili ‘moja, tunasaidiana. Utumishi wetu tunaupenda na twasaidiana. Twasaidiana sote, twasaidiana sote. Twamaliza kwa shangilio na kwa bidii kazi yetu.

 

2. Twafurahi kwa utumishi, hata tukiwa peke yetu; walakini heri zaidi kama tukisaidiana. 3.Ikiwezekana kwa mchwa ‘dogo kujenga kisuguu, sisi nasi kwa nguvu yake Mungu tutamaliza kazi.

 

4.Na umoja wetu ni wa thamani, unapendeza Mungu; anatubariki kwa neema, anatupa tunu kubwa.

 

5. Twakuomba, Bwana, ‘tuunganishe, tujaze pendo lako! Na kwa Roho yako utubatize, tuhudumie wewe!

A.L. Skoog, 1856-1935